TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Saturday, November 28, 2015

MSHTUKO KANISA PENTECOSTAL TANZANIA, MCHUNGAJI HUYU ASHANGAZA WENGI KWA NGUVU ZA KIROHO ALIZOKUWA NAZO, WAGONJWA WA UKIMWI, KISUKARI WAPONA LIVE, NI MAMBO YA KUSHANGAZA..!

 Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo Amos Mbena akifanya yake kwa mmoja wa waumini waliofika kwenye Kanisa lake wiki iliyopita na kushangaza wengi kwa nguvu ya ajabu aliyokuwa nayo.














 Na Mwandishi Wetu wa maskanibongo- Kimara
Maombi yanayoendelea kwenye Kanisa la Pentecostal Holness Mision Bonde la Ukombozi  lililopo Kimara Suka mtaa wa Gorani yamezidi kuwakomboa watanzania wenye mardhi sugu huku Mungu wa kweli akionekana live maeneo hayo kwa miujiza aliyowapa watumishi wake.
Kanisa hilo ambalo ni la miti kama linavyoonekana lakini linafanyakazi kubwa na ya kushagaza kwa watanzania watu wanapona live bila logo longo huku wakiondoaka na mibaraka tele.
Watu mbalimbali waliokuwa wamefrika wiki iliyopita ndani ya Kanisa hili wakiwemo waandishi wa habari walishuhudia uponyaji wa ajabu ambapo kuna watu walikuja na magongo wakatoka wakitembea wenyewe huku magongo hayo wakiyaacha kanisania hapo.
 
Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo  Amos Mbena aliuambia mtandao huu kuwa" Ndugu waandishi wa habari kama mlivyojionea hapa vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, watu wenye maradhi sugu yakiwemo Kisukari, Ukimwi na magonjwa yote ya ajabu wanapata kupona hapa hapa" Alisema Mchungaji huyo mwenye nguvu za ajabu 
Mchungaji huyo ambae nguvu zake zimezdi kiwanga kiasi kwamba kila akimuangalia mtu mwenye maradhi humgungua tatizo lake.
Hata  hivyo mchungaji huyo aliendelea kutoa uwito kwa sasa bado wanaendelea na uparesheni tokomeza magonjwa sugu hivyo watanzania watumie nafasi hiyo kupokea uponyaji wa matatizo yao ya aina yoyote na huduma yake hata ukimpigia kwenye simu atakufanyia huko uliko hata ukiwa Ulaya lakini kwa wakazi wa Dar wanaweza kufika Kanisani kwake Kimara Suka na watamuona Mungu wa kweli.
Mchungaji huyo alizitaja namba zake za simu kuwa ni  +255 716 200 065, ya Mchungaji Kiongozi Amosi Mbena  +255 657 897  211 ya mwinjilisti Inocent Gelvas na watapata uponyaji wa haraka

Friday, November 27, 2015

MASKINI YA MUNGU WEEH: MKUU WA WILAYA KINONDONI AFANYIWA UMAFIA WA KUTISHA, RAIS MAGUFULI, WAZIRI MKUU WAOMBWA KUMSAIDIA HARAKA ILI KUNUSURU UHAI WAKE. MASKANIBONGOTZ YANASA TAARIFA HII NYETI YA KUSIKITISHA!


Rais Dokta John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu wa Tanzania Mh Majaliwa Kassim Majaliwa ambapo viongozi hawa wakuu wameombwa na wananchi kumuongezea nguvu Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda ili afikie malengo yake ya kumaliza mgogoro huo wa Ardhi kwa amani huko Kata ya Wazo kwenye vitongoji vya Nakalekwa na Nakasangwe. Kwani changamoto kubwa aliyonayo Mkuu huyo wa Wilaya inadaiwa kuwa kwenye mgogoro huo yuko Kigogo mmoja mzito mwenye mamlaka kuliko yeye aliye upande wa mafisaidi. maskanibongotz
Mlinzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni akisogea karibu na mlango kwa ajiri ya kmufungulia ili aishuke kwenye viwanja vya Nakalekwa CCM siku ya jana tarehe 26.. maskanibongotz
                               
Mh Paul Makonda . maskanibongotz

Hii ndiyo shughuri aliyokutana nayo Makonda jana huko Nakalekwa  maskanibongotz



Hapa DC huyo akiwaombea msamaha kwa kuhiswa vibaya watumishi hao na kuwahisi watu wamesiwe na shakana kuhusu zoezi hilo kuwa litakwenda vizuri kwa baraka za Mungu. maskanibongotz


Na Mwandishi wa maskanibongotz
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kushtua, Hali ya usalama ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mheshimiwa Paul Makonda kwa sasa huenda ikawa mashakani baada ya kujitoa muhanga kupamba na ufisadi mkubwa unaofanywa na matajiri wenyewe mgogoro wa ardhi na wananchi wanyonge kwenye Kata ya Wazo mtaa wa Nyakasangwe na Nakalekwa, huku nyuma ya matajiri hao kuna vigogo wakubwa wa Serikali wenye nguvu kuliko yeye.
Habari za uhakika toka kwa vyanzo vyetu makini ambavyo havina hata chembe ya shaka viliuleza mtandao huu wa maskanibongotz kuwa Mkuu huyo wa Wilaya ambae amekuwa mstari wa mbele kutetea wanyonge hasa wanaoonewa kwenye masuala haya ya ardhi lakini mtihani mkubwa uliopo ni nguvu ya pesa kwani mafisadi wamewakamata watu wa mipango miji Manspaa ya Kinondoni, Watu wa Ardhi na hata msaidizi wa Dc huyo.
Mkuu huyo wa Wilaya wiki hii tarehe 25 mwezi huu ilikuwa anye mkutano na wakazi hao wa Nakasangwe na Nakalekwa ilikuwa kwa ajiri ya kuwaeleza wakazi hao namna alivyofanya jitihada za ziada kufanya vikao na pande zote mbili yani viongozi wa Serikali ya mtaa huo akiwa na kamati iliyokuwa imeteuliwa kwa ajiri ya kusimamia  vikao vya usuruhishi lakini pia timu ya pili ni ile ya watu wanaodai kuwa maeneo hayo wanayoishi wananchi ni yao.
Hata hivyo vikwazo vilianza kuingia baada ya Mkuu huyo wa Wilaya kufika kwa muda mrefu huku akiwasubiri maafisa Ardhi ambao walidaiwa walikuwa wametokea kwenye kikao cha siri na mafisadi hao kwa lengo la kukwamisha zoei hilo lisiende sawa kama lilivyokuwa limepangwa ambapo baadae walipofika maafisa hao kumi na moja Dc huyo aliamuru kuwaweka ndani kwa uzembe walioufanya lakini si hivyo inadaiwa mkuu huyo wa Wilaya nae alikuwa amepata taarifa za wapi walipokuwa wamepitia.
Kwa siku hiyo ya tarehe 25 zoezi hilo lilikwamba ambapo Mkuu wa Wilaya alimuagiza Mwenyekiti wa Nakasangwe Peter awaombe radhi wananchi kwa niaba yake kwa tukio lililokuwa limetokea na kuahidi zoezi hilo kuendelea kesho yake ambayo ni jana tarehe 26.
Hata hivyo siku hiyo ya jana wakazi hao zaidi ya elfu 30 walikusanyika mapema sana kwa ajiri ya kumsubiri Mkuu huyo wa Wilaya ili wamsikilize ambapo mapema tu kiongozi huyo anaechukia rushwa alifika akiwa ameongozana na wale maafisa Ardhi na watu wa mpango miji, Rpc Wambura na wale watu wa upande wa pili wanaodai maeneo hayo ni yao.
Baada ya kufika  eneo la uwanja wa CCM Nakalekwa Mkuu huyowa wilaya alikutana na mabango yenye jumbe za kushtua ambapo mabango hayo yaliyokuwa yanasema kuwa wakazi hao hawana imani na watu wa mipango miji kwa vile kuna taarifa wanashirikiana na  mafisaidi, huku pia wakazi hao wakimkataa moja kwa moja DASI msaidizi wa Mkuu wa Wilaya kwa madai kuwa yumo kwenye mtandao wa  kushirikiana na mafisadi hao ili wawadhurumu wakazi hao ardhi yao.
Sehemu hiyo mabango pia ili muomba Rais Dokta John Pombe Magufuli kuwashughurikia watu wa Mipando Miji na maafisa Ardhi kwa ufisadi na mambo mengine mabango hayo kama yanvoonekana pichani, hata hivyo hali hiyo ilimshtua Mkuu huyo wa Wilaya na kuwasihi wakazi hao kuwaamini maafisa ardhi wake kwani nay eye atakuwepo kwenye zoezi kwa siku za awari jambo ambalo lilipingwa vikali na wakazi hao kwa kuonesha wasi wasi wao kuwa endapo wakiachiwa maafisa ardhi hao peke yao bila yeye Dc huenda zoezi hilo lingeleta utata na ndichp kilichotokea leo tarhe 27.
Zoezi hilo kwa jana alilienda swa kwa vile Mkuu wa Wilaya alilisimamia vizuri lakini siku ya leo tarehe 27 zoezi hilo limeshindwa kuendelea baada ya watu wanaodaiwa kuwa ndiyo wenye mashamba ambao kwa awali walikuwa hata 20 hawafiki lakini siku ya leo wameongezeka na kufika zaidi ya 60 huku wakitaka nao waorozeshwe kwenye uhakiki wa viwanja hivyo.
Hali hiyo ikatibua mambo kwani japo la wajumbe wa nyumba kumi wakiongozwa na mwenyekiti Peter waligoma matakwa ya upande huo wa pili kutaka kupachikwa watu hao ambao hwatambuliki, lakini hata hivyo katika hali ya kushangaza maafisa Ardhi hao wakiongzwa na Seif walikuwa wanalazimisha watu hao wasiofahamika wawekwe tu ili zoezi liendelee.
Msimamo mkali wa mwenyekiti wa Serikali za mtaa na kamati yake kuwakataa watu waliokuwa wamepandikizwa ndiyo umepelekea watu wa ardhi kuchukia pamoja na wale wa upande wa mafisadi kuamua kuondoka eneo la viwanja hivyo na kupelekea zoei la uhakiki kusimama kuanzia leo hadi wananchi hao watakapotangaziwa tena.
JUHUDI ZA MAKONDA ZINAVYOKWAMISHWA NA KIGOGO MWENYE NGUVU KULIKO YEYE.
Katika jitihada za mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kuhakikisha mgogoro huo unamalizika kwa amani na isitokee tena watu wakauna kama katika eneo hilo zinadaiwa kukwamishwa na mtandao mkubwa ulimzunguka Makonda ambao ukiongozwa na Mkuu wake wa kazi mwenye nguvu kuliko yeye huku akiwapa nguvu watu wa Mipango miji, maafisa Ardhi, pamoja na msaidizi wake ambae wakazi hao wanasema hawataki kumuona kwa vile wanajua kila kinachoendelea kuhusu mgogoro huo.
Changamoto nyingine anayokutana nayo DC huyo ni kwamba mgogoro huo ameukuta unaendelea na mbaya zaidi baadhi ya watumishi wa Manisptaa wenye kitndo cha Ardh na Mipango miji wamekuwa sehemu ya mgogo huo na inadaiwa walishavuta pesa ndefu toka kwa mafisadi hao ili kuhakikisha wanapata eneo hilo kwa nguvu yoyote.
Bahari zaidi toka kwa vyanzo hivyo viliendelea kuueleza mtandao wa maskanibongotz kuwa  maafisa hao wanatajwa kwenye kashfa hiyo wametokea kumchukia DC MAKONDA kwa kitendo chake cha kuonesha kuwatetea wakazi hao  hali inayopelekea kushindwa kumpa ushirikiana na kama wanampa basi kwa shingo upande, na mbaya zaidi yupo kigogo mmoja ambae ana sauti kuliko Makonda kutokana na  kuwa karibu na mafisaidi hao wanaodaiwa kumwaga pesa kama mchanga.
Hali hiyo sasa inapelekea zoezi hilo kuwa na ugumu kutokana na maafisa mipango na Ardhi kulindwa na boss wake Makonda, hata hivyo wakazi hao wa NAKALEKWA na NAKASANGWE walionesha wasi wasi wao na hali ya usalama wa Mkuu wao wa Wilaya juu ya jambo hili kwani tayari kwa sasa Dc huyo yupo kwenye vita kubwa kupambana na boss wake, watu waliochini yake na mafisadi/
Kufuatia hali hiyo wananchi mbali wanaofatilia mgogoro huu wa kipindi kirefu wamemuomba Rais Dokta John Pombe Magufuli kumuongezea nguvu DC Makonda kwenye sula hili kwa vile hali ya usalama juu ya jambo hili kwa sasa kuwa mbaya kwani mkuu huyo anapambana hadi na bosi wake kikazi ambae anadaiwa kuwapa nguvu watu wa ardhi na mipango miji kuhakikisha wanakwambisha hili jambo.
Habari zaidi zilisema kuwa hata siku Makonda alipowaweka ndani watu hao wa Ardhi kwa amri ya kutowaachia hadi kwa amri yake dakika chache baadae ilidaiwa boss wake Makonda alipiga simu na kuamuru waachiwe haraka maafisa ardhi hao.
Kigogo huyo pia amewahi kusababisha mgogoro wa watu wa gereji pale Tegeta kwa kutaka kuwahamisha watu hao hali iliyozusha balaa kubwa kwani kigogo huyo ana rafiki yake muhindi ambae ndiye aliyekuwa anapataka pale kwa watu wa magereji si kama alivyokuwa ametangaza kuwa wamevamia eneo la hifadhi.
Mtandao huu unaungana na watanzania wapenda amani, wapenda haki kuiomba Serikali Kuu kwa maana ya Waziri Mkuu , Majaliwa Kassim Majaliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimwa Dk John Pombe Magufuli kusikia kilio cha wapiga kura wake, lakini pia kuchunguza tuhuma hizi zinazowakabiri maafisa Ardhi, Mipango Miji na msaidizi wa DC Kinondoni ili kama zina ukweli ndani yake basi wachukuliwe hatua haraka ili kuepusha uvunjifu wa amani.
Mwandishi wa maskanibongotz  siku ya aleo alifika ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kinondoni kwa ajiri ya kuzungumza na Mkuu huyo wa Wilaya kuhusu changamoto hizo na tuhuma zinazowakabir maafisa wake wa ardhi na mipango miji hadi wananchi kuwakataa lakini mkuu huyo hakuwepo ofisini na tulielezwa yupo nje ya ofisi kwa kwa majuku ya kiofis.
Credit:maskanibongotz

Monica kamuweka Akon kwenye hii mpya; ‘Hustler’s Ambition’ na angependa ikufikie – (Audio)


Msanii wa muziki wa R&B kutoka Marekani, Monica Brown maarufu kama Monica ataachia Album yake ya nane Code Red tarehe 18 December 2015… na baada ya kuachia single inayobeba Album hiyo na Missy Eliott, Monica amerudi tena kuweka headlines na single nyingine kutoka kwenye Album hiyo.
MONIAKON2
Wimbo unaitwa ‘Hustler’s Ambition’ na feature ya wimbo huu imesimamiwa Mkurugenzi wa Konvict Muzik, Akon… Ukiachia mbali single aliyofanya na Missy Eliott na hii mpya na Akon, Album ya Monica, Code Red imebeba featuring za wasanii kama Timbaland, Polow Da Don na Lil Wayne ambaye alionekana kwenye video ya Just Right For Me.
MONIAKON3
Hustler’s Ambition ni mdundo wa daika nne tu mtu wangu, kuunasa bonyeza play hapa chini.

Thursday, November 26, 2015

JARIBU LA KWANZA TANGU AAPISHWE: WATUMISHI MANISPA YA KINONDONI WAMCHOKONOA PABAYA RAIS MAGUFULI, DC MAKONDA APINGWA VIKALI, APOKEWA NA MABANGO YA KASHFA MBAYA, PICHA HIZI HAPA…!

 Hivi ndivyo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni alivyopokelewa na mabango ya kuwakata watumishi wa Kitengo cha Ardhi kwa madai ya kushirikiana na mafisadi wanaonea wananchi kwenye mgogoro huo wa ardhi eneo la Nyakasangwe na Nakalekwa leo hii asubuhi.maskanibongotz
Rais John Pombe Magufuli ambaeombwa na wananchi hao walioteseka kwa miaka mingi na mgogoro wa ardhi kumuongezea nguvu DC MAKONDA kwa madai ya kuwatuhumu watu wa kitengo cha ardhi kushirikiana na mafisaidi kuhujumu ardhi hiyo.

 Mapema leo wakazi hawa wakiwa Nakalekwa CCM wakimsubiri Mh Paul Makonda


 Mabango yaliyokuwa yanampongeza Dc Makonda kwa kujito muhanga kupambana na mafisadi ili kuwatete wananchi hao wanyonge 





 Dc akiingia eneo la uwanja wa Nakalekwa kwa ajiri ya kuzungumza na wakazi hao tayari kwa ajiri ya kuanza zoezi la kuhakiki viwanja vyao ili baadae wapimiwe na kumaliza mgogoro huo ulimshinda Dc aliyemtangulia na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni wa sasa.
 Mh Makonda akipokelewa na mabango kama hivi





 Mh Makonda akishangaa mabango mbalimbali yaliyokuwa na ujumbe tofauti kama yanvyoonekana

Moja ya bango linasomeka hatumtaki  DASI ambae ni msaidizi  wa DC Makonda ambae anatuhumiwa kushirikiana na mafisadi hao kuhujumu wananachi,



Na Mwandishi wetu- Nakasangwe WAZO
Katika hali isiyokuwa ya kawaida leo hii bila hekima na kauri nzuri za Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda kwa wakazi wa Nakasangwe na Nakalekwa waliopo kata ya Wazo wenye mgogoro wa ardhi basi huenda tungeripot tofauti habari kutokana na ghazabu kubwa waliyokuwa nayo wananchi ya kuwakataa watu wa mipango miji, Maafisa Ardhi, na Msaidizi wa Mkuu wa Wailya Mheshimwa Dasi wasishiriki zoezi la kuhakiki viwanja vyao.
Mwandishi wa Maskanibongotz aliyekuwepo eneo la tukio amesema kuwa hali ilikuwa mbaya baada ya wakazi hao kuibuka na mabango yenye kumuomba Rais Magufuli amuongezee nguvu Paul Makonda kwa vile kwenye zoezi hilo ni kama yupo peke yake kwani karibia watumishi wote walitajwa kudaiwa kuhusika na rushwa toka kwa mafisadi hao.
Wakizungumza na maskanibongotz watu hao walisema " Jamani Makonda amejitoa muhanga lakini hana sapoti hivyo kupitia nyie waandishai wa habari tunaomba mfikishie ujumbe wetu Mheshimiwa Rais Magufuli kuwa tunamuombsa amuongezee nguvu Makonda kwani hapa amezungukwa na wasaliti watupu sisi tunajua kinachoendelea" Walisema watu
Aidha watu hao walisema hata jana kitendo cha maafisa Ardhi hao kuchelewa kulikuwa na namna ambapo indaiwa walikuwa na kikao kingine na mafisadi hao na kuna taarifa kuwa pia kuna nyaraka za ardhi wameshawatengezea mafisadi hao ili kuwakandamiza wao.

Baada ya Mkuu huyo wa Wailaya kuona jazba za wakazi hao alilazimika kutumia maneno yenye hekima na busara pamoja na kuwaomba wakazi hao wasijari yeye mwenyewe yupo na atashiriki siku mbili kisha atawaacha watumishi hao waendelee na pia wakazi hao wawaamini watumishi wake.

Wakazi hao walikubari kwa shingo upande lakini bado walizidi kumuomba Mh Rais amuongezee nguvu Makonda kwa vile kwa sasa yupo kwenye wakati mgumu kutokana na kuzngukwa na wasaliti kwa madai hayo ya kuwabeba mafisaidi wanaotaka kuchukua eneo kubwa hukuwakazi hao elfu mbili na mia tano waachwe bila makazi jambo ambalo hata kwa Mungu halina baraka.
Aidha wakazi hao wamempinga Mhe Makonda kuwaacha watumishi hao peke yao kusimamia zoezi hilo kwani tayari wanatuhuma za kushirikiana na mafisadi, huku wakisisitiza Rais Magufuli amuongezee nguvu.
Hata hivyo kwa madai hayo ya wakazi hao kuwatuhumu watu nwa ardhi, Mipango Miji na Msaidizi wa Makonda kuwa watuhumiwa kwa ufisaidi wananchi mbalimbali wapenda amani wamemuomba Rais kupitia ujumbe wa wananchi kufanya uchunguzi wake kama alivyoahidi siku alipolihutubia bunge Dodoma kuwa kwa mtumishi yeyote atakaebainika kwa ufisaidi ama rushwa na ushahidi ukiwa sawa basi watimuliwe hivyo basi angeanza kwa maafisa hao.
Credit: maskaningotz
 


Wednesday, November 25, 2015

BREAKING NEWS: DC MAKONDA KAMA RAIS MAGUFULI VILE, AWAWEKA NDANI MAAFISA ARDHI KINONDONI UNATAKA KUJUA NINI KILICHOWAPATA? MASKANIBONGOTZ LINAKUPA ISHI NZIMA..!

 Mwenyekiti wa Nyakasangwe kata ya Wazo leo hii akitangaza kwenye kiwanja cha CCM Nakalekwa juu ya Mh Paul Makonda kushindwa kufika baada ya maafisa Ardhi waliokuwa waje kuendesha zoezi la kuhakiki ardhi za wakazi hao na mafisaidi baada ya DC huyo kuamuru kuwekwa ndani kwa muda usiojulikana maafisa ardhi hao kwa kuchelewa kufika kwenye majukumu yao huku maelfu ya wananchi wakifika tangu saa kumi na mbili asubhi. visit maskaningotz

Maelfu ya wananchi wa Nakalekwa na Nakasangwe wakiwa viwanja ya CCM Nakalekwa wakimsubiri Mh Paul Makonda leo asubhi. Picha zote kwa hisaani ya mtandao wa maskanibongotz










 

























 Hivi ndivyo maelfu ya watu waliokuwa wanamsubiri Mh Paul Makonda na baadae kushindwa kutokea hali iliyowafanya wananchi hao kuwaghazabika





Na Mwandishi wa Maskanibongotz aliyekuwepo eneo la tukio.
Hata kama kusoma hujui hata picha kutizama? Hakika anaebisha acha abishe Tanzanani ilikuwa inahitaji viongozi kama akina DC Mkonda na Rais Mgufuli kiukweli kama mwendo huu utakuwa hivi basi Tanzania mpya hiyo inakuja tena miaka miwiki ijayo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambae jana tu ametoka kuzungumza na maafisa wote wa Wilaya yake kuhusu kujituma kazini badala ya kusukumwa hatimae Paul Makonda leo amewatia ndani maafisa Ardhi wake wawili baada ya kuchelewa kufika kwenye majukumu yao.
Tukio hilo lililowaacha watu midomo wazi huku wakimpongeza DC huyo limetokea eneo la Nyakasangwe Serikali za mtaa ambapo leo hii kulikuwa na zoezi la uhakiki wa viwanja vya wakazi  na Nakasangwe na Nakalekwa huku maafisa Ardhi hao wakiwa wasimamizi.
MAKONDA AKASIRIKA:
Mkuu huyo wa Wilaya akiambatana na RPC Wambura wa Kinondoni, Ocd Kawe, gazri za Polisi na baadhi ya mafias usalama walifika mapema eneo hilo kama saa tano na moja kwa moja walifikia Serikali za Mtaa  wa Nyakasangwe na kupokelewa na Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa huo.
Hata hivyo  wakati msafara huo wa Dc ukiwa Serikali za mtaa wa Nyakasangwe upande wa Nakalekwa tayari kulikuwa na umati mkubwa wa watu waliokuwa wanamshubri Mh huku wakiendelea kuungua jua kali.
Habari zaidi zilisema DC huyo akiwa bado Serikali za mtaa alisikika akimpigia simu Mkurugenzi wa Manispaa akimta angalizo kuhusu vijana wake wa kazi kwa nini wanakuwa wazembe kiasi hicho yani wananchi toka saa kumi na mbili wapo kwenye maeneo yao huku maafisa ardhi hao ambao ndiyo watu muhimu kwenye utekelezaji jukumu hilo wakiwa bado hawajafika.
Hata hivyo baada ya dakika kadhaa maafisa ardhi hao walifika wakiwa wanatetemeka  ambapo moja kwa moja Mh Paul Makonda akamuamuru OCD Kituo Cha Kawe kuwaweka ndani haraka huku akimuomba Mwenyekeiti wa Nyakasangwe kuwaomba radhi wananchi kwa dharura hiyo hadi hapo kesho saa mbili asubuhi.
Akithibitisha kutokea tuko hilo Mwenyeketi wa Nyakasangwe pichani akiwahutubia tuki maelfu ya wananchi hao na kuwaeleza kuhusu tukio hilo na kuahirisha zoezi la uhakiki viwanja hivyo kabla ya kupimiwa.
Hata hivyo katika hatua  nyingine wananchi hao wamemuomba DC Makonda kama kweli anataka kutafuta amani kwenye eneo hilo ili kumaliza mgogoro awe makini na upande wa mafisadi kwani kwa kitendo kilichoonekana leo cha kuwaleta watu wengi wasio husika ambapo ni janja ambayo watu hao wameamua kuifanya baada ya kuonba upepo mbua unawalemea wameamua kuwatengeneza watu ili waonekane hayo maeneo ni yao kukwepa kuonekana kuwa na eneo kubwa.
Wakazi wengi wa eneo hilo tayari wako kwenye vipanda vyao wakiishi na familia zao hivyo wale wote waliopo kwenye nyumba waachwe kama walivyo kwa vile tayari wameshatumia gharama nyingi kujenga maeneo hayo.
Mtandao huu wa maskanibongotz unampongeza DC huyo kwa juhudi za kutafuta amani ambapo Mungu aendelee kumuongoza ili awasaidi watanzania wenzetu hao ambao ni wanyonge wanaopigana na wenye nguvu ya pesa.

Credit:maskanibongotz