NEW MAISHA CLUB

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0715780495 NA 0767575718 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Monday, May 20, 2013

NEY WAMITEGO NA DIAMOND WAFUNIKANA MBAYA KWENYE UZINDUZI WA VIDEO YA MUZIKI GANI













Ney wa Mitego akiwarusha wapenzi wa burudani.

Nyomi iliyoitikia shoo hiyo.


Diamond na Ney wakiwapagawisha mashabiki.

Ney wa Mitego akisema na wapenzi wake.

Diamond Platnumz akionyesha umahiri wake stejini.


Diamond akifanya makamuzi sambamba na kundi lake.

Ney wa Mitego akilishambulia jukwaa la Dar Live.

Mashabiki wakiburudika wakati wa shoo hiyo ndani ya Dar Live.

Diamond na kundi lake katika pozi kabla ya makamuzi.

DAR Live usiku wa kuamkia leo ilitikisika baada ya mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia onyesho la pamoja kati ya wanamuziki wawili nyota wa kizazi kipya, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Ney wa Mitego ambao walikuwa wakizindua video ya wimbo wao wa 'Muziki Gani'.
Wanamuziki hao kwa pamoja walitoa burudani ya nguvu ambayo ilizikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika ukumbi huo wa maraha uliopo Mbagala Zakhem, jijini Dar.
PICHA ZOTE NA  http://audifacejackson.blogspot.com/

Sunday, May 19, 2013

MWALIMU WA CHEKECHEA ANASWA KWA UTAPELI,ANUSA KIFO KWA KIPIGO!

Tapeli hatari aliyefahamika kwa jina la Baba Kisiva akiwa ametapakaa damu baada ya kipigo toka kwa wananchi wenye jazba.

Tapeli akieleza kuwa yeye ni mwalimu wa shule za moja ya Chekechea Mkoani Arusha. Nakuomba asamehewe kwani alichokifanya ni njaa tu.



Wananchi wakimfunga kamba baada ya kumuokoa tapeli huyo aliendelee kupigwa na wananchi wenye hasira baada ya kutapeli laki nne kwenye duka la M PESA.





Wananchi wenye jazba wakiwa nje ya duka hiyo huku wakimuomba mwenye duka kumtoa nje tapeli huyo ili waendelee kumuadhibu.

  Baba Kisiva akiendelea kumuomba mwenye duka asimtoe nje wananchi wasije kumuua kwa kipigo
Begi alilokuwa nalo tapeli huyo likiwa na kisu pamoja na viwembe mbalimbali kwa ajili ya kudhuru watu.


Alitapeli  laki nne kwenye kibanda cha Tigo Pesa.Anusurik kifo kwa kipigo.
Na Livingstone Mkoi

Kijana mmoja ambae inadaiwa ni tapeli hatari Jijini Dar es Salaama aliyefahamika kwa jina la Baba Kisiva ambae anatokea Muarusha wiki iliyopita alinusurik kifo baada ya kutapeli shilingi laki nne dukani kwa mangi.

Tukio hilo la aina yake lilitokea maeneo ya Kinondoni Mkwajuni karibu na baa ya Maridadi “ Makao Makuu” na kushuhudiwa na mamia ya wananchi huku akiponea chupu chupu kuchomwa moto na wananchi wenye jazba kubwa.

Akiongea na Xdeejayz Wakala wa huduma za kurusha pesa kulikofanyika tukio hilo aliyejitambulisha kwa jina la Gradstone Fanuel alianza kumueleza mwandishi wetu kuwa kijana huyo alifika dukani kwake na kumtaka amrushie shilingi laki nne kwenye simu yake haraka.

Hata hivyo kutokana na kutomtilia shaka mteja huyo wakala huyo alifanya kama mteja wake alivyohitaji.Baada ya kufanikisha kutuma pesa na meseji kuonesha kuwa pesa ilitumwa kwenye simu namba 0755-689171 na kuonesha jina la mtu aliyepokea pesa hiyo kuwa ni Dokta John Katoko.

Aidha baada ya kumuonesha mteja wake hiyo iliyosomeka kuwa “Q56EI038 imetumwa kwa DOKTER JOHN tarehe 9/5/13 saa 5:44 PM Salio lako….. Tsh……” Ambapo mteja wake alianza kuingiza mkono mfukoni ili kutoa pesa kiasi hicho cha shilingi laki nne.

Hata hivyo muda ulizidi kwenda huku hakuna matumaini ya kutoa huyo pesa huku akionekana kupiga mahesabu ya kumkimbia wakala huyo ambae ni maarufu maeneo hayo ambapo haraka aligundua kuwa mteja wake huyo alikuwa tapeli ndipo wananchi walianza kumtia adabu.

Aidha katika hali isiyotarajia dakika moja tu baadae iuligundulika pesa hiyo ilikuwa imeshatolewa kwenye simu namba  Dodwin Listen Godwin hasa baada ya kuulizia makao makuu ya mtandao husika.Baada ya kibano kikali toka kwa wananchi huku wakimtaka kijana huyo kujieleza kuwa anatokea watu ndipo alisema kuwa anatokea Mwananyamala lakini ni mwenyeji wa Arusha na kule yeye ni mwalimu wa shule moja ya Academi ambayo alishindwa kutaja jina.

Hata hivyo kijan huyo aliwashukuru madalali wenye ofisi karibu na dula la wakala huyo ambao walimsaidia kumuokoa na kumuingiza dukani kwa aliyetapeli hadi polisi walipofika kumuchukuwa na kumpeleka kituo cha Oysterbay kasha kumfungulia jarada OB/RB/8212/ UWIZI WA PESA KUTUMIA MTANDAO.

Imeelezwa kuwa vijana hao wako sita hivyo wakati wa kwenda kutapeli hujipanga wawili wawili kwa ajili ya kufanikisha zoezi hilo la utapeli hivyo inadaiwa wameshawaliza watu wengi sana hivyo wakazi wa Jijini wameliomba jeshi la Polisi kuwachukulia hatua kali wale wote wanaokuwa wanakamatwa kwa makosa hayo ili kukomesha matukio hayo.

GOLI LA DIDIER KAVUMBAGU KWA SIMBA NUSRA LIMTOE ROHO JB,AONDOKA MAPEMA UWANJANI!


 Msanii JB kulia akiwa na Masanja Makandamizaji

 Msanii JB kulia

 Msanii JB kulia ambae ni shabiki mkubwa wa timu ya soka ya Simba, Huku akiwa amevalia tisheti ya timu hiyo.

Na Livingstone Mkoi

Katika hali isiyokuwa ya kawaida goli la dakika ya nne lililofungwa na mchezaji Didier Kavumbagu dhidi ya Simba nusra limtoe roho msanii nyota wa filamu za Kibongo Jb ambae ni shabiki wa Simba.

Mapapalazi wetu waliokuwa wamesambaa kila viunga vya uwanja huo walimshuhudia JB ambae aliingia uwanjani hapa majira ya saa tisa na robo za jioni akiwa ameongozana na Shamsa Ford pamoja na wasanii wengine.

Aidha baada ya kufika uwanjani hapo kama kawaida akiwa amevalia uzi mwekundi pamoja na kitu chekundi alikwenda moja kwa moja hadi jukwaa la Simba na kukaa.

JB ambae awali alionekana kuwa mchangamfu na mwenye matuamaini ya ushindi kwa timu yake ambapo katika hali isiyotarajia mara baada ya mpira kuanza ndani dakika nne mshambuliaji hatari wa Yanga DIdier Kavumbagu aliiandikia tumu yake goli la kwanza baada ya  kupigwa kona.

Msanii huyo alijikuta anang'onyea kabisa na kupoteza uchangamfu,Hata hivyo hali ilikuwa mbaya baada Yanga kuongeza goli la pili kupitia kwa mchezaji wale Hamis Kiiza Jb alipoteza matumaini kabisa. 

MASHABIKI YANGA WALIOMTEKA MRISHO NGASA UWANJA WA TAIFA KUSHTAKIWA!

 Hapa mmoja wa mashabiki wa Yanga mwenye jezi namba 24 na wengine wakiwa wamemzingira Mchezaji wa Simba Mrisho Ngasa haonekani pichani.

Mrisho Ngasa kama anavyoonekana akiwa kwenye moja ya mechi za timu Taifa Jijini Dar hivi karibuni.

Na Livingstone Mkoi

Kitendo cha mashabiki wa timu ya Yanga cha kumteka mchezaji harari wa timu ya Simba Mrisho Khalufan Ngasa kimewakwaza baadhi ya wadau wa timu ya Simba mbapo kwa pamoja wamepanga kuwachukulia hatua mashabiki hao ambao walionekana kwa macho.

Wakiongea na Xdeejayz muda mfupi mara baada ya pambano kumalizika mashabiki toka Mkoani Morogoro wakiongozwa na Mudy Muthelezi walisema " Kweli sisi hatukuona haki kwa mashabiki wa Yanga kumteka Ngasa na kumzungusha kwa uwanjani na kama ikithibitika Ngasa mwenyewe akikili alifanyiwa hivyo bila idhini yake tutachukuwa hatua kali kwa kuwashtaki mashabiki hao walimfanyia hivyo" Alisema Mudy ambae pia ni dalali mkubwa wa magari Mkoani humo

 

MASHABIKI WA SIMBA: KWA MUZIKI WA YANGA ISINGEKUWA RAHISI SIMBA KUEPUKA KIPIGO!

 Wachezaji wa Yanga wakiwapa mikono wachezaji wa Simba muda mfupi kabla ya mchezo ulipigiwa jana jioni kwenye uwanja wa Taifa.


 Wachezaji wa Yanga Didie Kavumbagu nyuma yake kulia Hamisi Kiza wakishangia kwa staili ya kuwashukuru mashabiki wao wa Yanga

Golikipa wa Simba na Captain wa timu Juma .K. Juma hiyo akiwa hoi kwenye eneo lake baada kuumia vibaya kufuatia mpira wa adhabu iliopigwa na Nizar Khalufan ambao uligonga mwamba.


 Jerison Tegete akiwa na Kocha wa Simba Julio kwenye moja ya matukio uwanjani hapo yaliyokuwa yananaswa na kamera hatari na za kisasa za DVT/ Xdeejayz.



 Mtangazaji wa DTV kupitia kipindi cha X-Africa  Dakota mwenye miwajini ta tisheti nyeusi akiwa kwenye jukwaa la mashabiki wa Yanga kufatilia pambano hilo lililokuwa na vibweka kibao.


Mwali Live uwanjani.


 Aaga! Aaga! Aaga! cheza kiduku ndivyo wachezaji wa Yanga walivyokuwa wanaimba muda mpufi baada ya mwamuziki kupuliza kipyenga cha mwisho.

 Didier Kavumbagu katikati akiwaongoza wachezaji wenzake kucheza sebeni uwanjani hapo kufuatia timu yao kuifunga Simba jumla ya mabao 2-0 na kukabidhiwa Kombe la Ligi Kuu Tanzania Bara 2013/14

PICHA ZOTE NA LIVINGSTONE MKOI ALIYEKUWA UWANJANI



Friday, May 17, 2013

NEY WAMITEGO AJITAMBA KUMKALISHA DIAMOND PLATNUM

Katika hali ya Amani kimuziki Msanii Nay wa Mitego amemrushia vijembe Msanii mwenzake
Diamond Platnumz Jionii ya Leo......''
Niliamua kumwendea hewani Nay wa Mitego Kujua kajianda vipi 
kuhusiana na Show ya kesho
Usiku Darlive......Na Mnukuu Nay wa Mitego akifunguka
 baada ya swali aliloulizwa,
Nay''Napenda kumwambia bwana mdogo Diamond kuwa kesho
akae tayari kwa kuwa naenda kuandika
Historia Mpya Darlive,Nataka watanzania wote wajitokeze waje
 kuona navyomkalisha mbana pua
na wavaa nguo za dada zao wanaojidai kwenda sawa na utandawazi......''
Nay alizidi kufunguka kuwa kesho ndo utakuwa mwisho wa 
Diamond na kumthibiishia
kuwa Hip Hop ndo muziki unaolipa na wenye maana zaidi......!!

Hayo ndo maneno aliyoyatoa Nay dakika chache zilizopita 
alivyopigiwa na Mwandishi wa This Is Diamond
Kuhusiana na Show kubwa kesho Darlive......

Stay Tuned Nitamuenda Hewani The Kid From Kigoma baada ya 
kumfikishia ujumbe huu wa Nay...
Je maneno hayo kakubaliana nayo....?
 Stay here kusubiria jibu la Diamond Juu ya ujumbe huu.....!!

SPORT LIVE YA DTV KESHO JUMAMOS LIVE KWENYE PAMBANO LA SIMBA NA YANGA UWANJA WA TAIFAI!

OREST KAWAU MMOJA WA WATANGAZAJI WA KIPINDI CHA MICHEZO DTV.

Na Livingstone Mkoi

Timu ya wananmichezo wa kipindi cha Sport Live kinachorushwa na Dar es Salaam Televisheni DTV kesho wanatarajia kushusha mitambo yao ndani ya uwanja wa taifa kwa ajili ya kufanya coverages nzima ya mapambano wa mechi ya watani wa jadi kati ya Simba na Yanga.

Akiongea na Xdeejayz Program meneja  wa DTV  Mathew Philip alisema " Kwa mara ya kwanza tutapeleka timu ya waandishi wetu kwenye pambano hilo huku wakiwa na kamera za kisasa kabisa ili kuchukuwa kila kinachoendelea uwanjani hapo" Alisema Mathew

Aidha kiongozi huyo aliongeza kusema kuwa " Tuliandika barua kwa ajili ya kuimba TFF kuwapa vitambulisho waandishi wetu ili waweze kufika uwanjani hapo siku ya kesho Jumamosi kwa ajili ya kutimiza majukumu yao na tayari TFF imeshatoa baraka tayari ya kupatiwa vitambulisho wanahabari wetu" Alisema meneja

Hata hivyo meneja huyo alimaliza kusema mashabiki wa michezo wanaombwa kuwa na subra tu lakini hivi pundi kuna suprise kubwa inakuja kwao kupitia DTV hasa kwa wapenda michezo yote ndani na nje ya nchi DTV NI WAKATI WAKO.

Aidha waandishi wa Xdeejayz nao watahakikisha wanakuwepo ili kuwaretea kila kinachoendelea uwanjani hapo ili kuwapa raha murua.